SAFARI YANGU YA WOKOVU
YESU ASIFIWE SANA... Nimekuwa nikikutana na jumbe za watu wakitaka niwaeleze niliokokaje? Nikashindwa kumjibu mmoja mmoja badala yake nikawa nikiwaambia nitawajibu siku. Leo ninalitimiza hilo. Kwa majina naitwa Annah steven Tewele, mwenyeji wa mkoa wa Iringa lakini kwa sasa naishi Dodoma kimasomo. Mama yangu Veronica Sanga aliokoka kitambo sana hata kabla hajaolewa. Enzi za ubinti wake alikuwa mtumishi wa Mungu mzuri hasa kwenye eneo la maombi. Mpaka akatuzaa watoto 4, mimi nikiwa second born, tangu udogo tulikukulia kwenye wokovu wa kurithi kwa mzazi (mama). Tusipoenda kanisani viboko, Hivyo tulikuwa tunakwenda vipindi vya watoto kila jumamosi na jumapili. Nikiwa darasa la tatu nilipata rafiki mle darasani ambaye alikuwa na kundi kama la watoto 5 hivi. Kila siku wanachanga hela (zamani hizo hela za kula shule ni 50 au 100), wakichanga watanunua miwa, vibama, mifudu na visheti kisha tunagawana. Mimi nilikuwa sipewi hela mara chache, hivyo nikienda shuleni bila hela we...