JINSI NILIVYOTAHADHARISHWA KABLA YA AJALI
"Rafiki yangu ambae ni mtumishi wa Mungu, alinionya sana juu ya kudharau ndoto. Alinisihi tuchukue hatua ya kuomba. Basi, tulichukua wakati tukafunga maombi.." YESU APEWE SIFA., Mimi ninafanya kazi ya UWAKALA wa mitandao ya simu yaani M-PESA, TIGOPESA, Airtel Money na HALOPESA. Siku moja nikiwa nimelala nikaota ndoto moja ambayo haikunifadhaisha sana na nikaichukulia kirahisi bila tija yoyote. “Tazama, nilikuwa katika kibanda changu nikiendelea na kazi yangu ya uwakala kama kawaida. Kibanda changu kilikuwa mtaani kando ya barabara. Nikiwa ndani ya kibanda, ilitokea gari likiwa kwenye mwendokasi wa ajabu kana kwamba limekatwa breki. Lilianguka na kuanza kubiringika kuja uelekeo wa kibanda changu hali nimo ndani yake. Kabla gari lile halijanifikia, nilishtuka kutoka usingizini.” Niliwaza lakini nikachukulia ni ndoto tu, na asubuhi nikaenda kuendelea na kazi kama kawaida. Siku moja wakati napiga storin a Rafiki yangu ambae ni mtumishi wa Mungu, alinionya s...