RAFIKI YANGU ASIYEONEKANA KWA MACHO
“Ndoto! ndoto! siku fulani nilipanga kuamka saa tisa alfajiri kuwa na mda na rafiki yangu asiyeonekana. ilipofika saa tisa juu ya alama nilishtuka. uchovu niliokuwa nao ulinifanya niendelee kulala. ndani ya dakika 37 za kulala huko niliota ndoto ifuatayo….”
YESU ASIFIWE.,
llikuwa
ni usiku mmoja mtulivu majira ya tisa alfajiri nikiwa narejea nyumbani
gafla niliona majitu mawili yenye nguvu yamevalia mavazi ya jeshi. bila
kujua kosa nililotenda amri ilitolewa nikalala chini kifudifudi na
kuchapwa viboko viwili. nikiwa pale chini nimelala pasi kujua hatima
yangu niliyaona yale majitu kama yakijadili kufanya ubaya flani. yakiwa
yamezubaa nilipata fursa ya kuyaponyoka na kutimua kuvumbi kuendeleza
safari yangu kuelekea nyumbani. nikiwa njiani nilipita njia iliyokuwa na
maziko na kumkuta mrimbwende mmoja amefichama kando ya mti.
alivyoniona
alianza nishutumu mimi kuwa sababu ya mambo yake yanayokwenda mkama.
nilivyomtaka athibitishe amejuaje kuwa mimi ndiye chanzo, alinijibu kuwa
amejuzwa na mtaalamu kuwa yeyote atakayepita eneo hilo mda huo ndiye.
alianza kukata tawi la mti kutaka kuniadhibu huku amegubikwa na jazba
kubwa.
angali katika jitihada zake za
kukwanyua tawi hilo la mti nilipata upenyo wa kutimua kivumbi tena
kuendelea na safari yangu. nikiwa katika mbio nilikigeuza kichwa changu
kutazama nini kinaendelea, macho yangu yakumuona yule mrimbwende akiwa
na mabinti wengine wawili wakinifukuza kwa hasira.
niliendelea kukata mbuga kuelekea nyumbani maana nilijua ndiko salama
yangu iliko. nikianza kuyaona mandhari ya nyumbani kwa mbali, nyuma
yangu wale warimbwende walikuwa wamenikaribia sana. gafla akatokea
mwanamume mmoja akawakamata wale mabinti wote kwa wakati mmoja.
masikioni mwangu kwa mbali nikawa nawasikia wakimsihi awaachie ili
waendelee kunifukuza. mtazamo wa sura yake kama alitaka kuwaachia.
nikapaza sauti yangu na kumsihi mwanamume yule nikisema usiwaachie mpaka
nitakapokuwa nimeingia mlango wa geti la nyumbani maana nimekaribia
sana. nikiwa na mashaka kama atafanya kama nilivyomsihi niligeuka na
kumwona kawakamatilia bado.
niliendeleza mbio zile kuelekea nyumbani. nilipoanza kuingia maeneo ya
makazi majira ya saa kumi alfajiri niliisikia sauti ikitoka redioni.
ilikuwa sauti ya mtu akiomba. sauti iliyosikika ilikuwa ya mtu akiomba
kwa bidii. miongoni mwa maombi aliyokuwa akiomba ni ulinzi wa Mungu kwa
watu wanaopita katika hatari mbalimbali.
niliendelea
kukimbia mpaka nikaingia mlango wa geti la nyumbani salama kabisa.
mwili wangu ulikuwa umechoka nikihema kwa nguvu sana.
ilikuwa furaha nilipogundua kuwa mlango wa kuingia ndani ya nyumba pia
ulikuwa wazi sikuhitaji kuita mtu kunifungulia. niliingia ndani nikiwa
salama kabisa. nilianza tafakari jinsi nilivyookoka na mikono ya watesi
wale gafla maneno ya kitabu cha Luka 22 yakaanza kunijia kichwani
mwangu. mstari wa 40 aliwaambia wanafunzi wake ombeni kwamba msiingie
majaribuni. ijapokuwa yeye alikuwa ni Mungu(mtawala) lakini mstari wa 41
unaonyesha mwenyewe akajitenga nao kama kiasi cha kutupa jiwe, akapiga
magoti akaomba. mstari wa 43 waonyesha msaada toka mbinguni ulishuka na
kumwezesha kusonga mbele salama katika kusudi la Mungu. 45 na 46
yaonyesha jinsi Yesu alivyopatwa na huzuni kuwakuta wanafunzi wamelala
hawaombi. akawasihi tena ombeni msije mkaingia majaribuni. kumbe
tukiomba msaada wapatikana na tunavuka salama.
USILALE, TUOMBE.
####################
JE, UNA USHUHUDA AMBAO UNGEPENDA TUUCHAPISHE??
Fanya hivyo ili maelfu wajue mambo ambayo MUNGU alikutendea na kupitia ushuhuda wako maelfu ya wasomaji watayashuhudia matendo ya Mungu uliyenaye.
Endapo unao Ushuhuda tafadhali BOFYA HAPA
Mungu Ni wa ajabu
ReplyDeleteNinakumbuka Sana jinsi Mungu alivyonitumia wakat ule mpaka sasa
ReplyDeleteAmina Ushuhuda mzuri Sana unanijenga Kwa kweli, Ubarikiwe sana
ReplyDelete